Kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu tulishindwa kuwapa mwendelezo huu. Sasa kaa mkao wa kula na hii ni sehemu ya 45.ENDELEAAAA..............
Wakati Siwema anafungua mlango ili atoke nje kabisa, ikasikika sauti“Mbona mapema sana, hata chai hujanywa?”
Wote wakatazamana kwani hakuna aliyeongea muda huo, katika kushangaa zaidi wakamuona yule mtoto mchanga akija sebleni.
Hakuna aliyeweza kustahimili jambo lile na kujikuta wakiinuka ili kuanza kukimbia ila walianguka chini, kisha yule mtoto akasogea kwa Siwema na kumvuta kwa ndani kwakweli Siwema alikuwa akitetemeka sana kwani alishangaa jinsi mtoto mdogo hivi alivyoweza kutembea na alivyokuwa na nguvu za kumvuta. Wote wakawekwa pale sebleni kisha yule mtoto akaanza kucheka na gafla akageuka na kuwa Neema,
“Yani nyie mmefanya kazi ya kunitafuta sana, hata sikuwa na shida ya kuwasumbua mapema hivi kwani mida yangu ni usiku ila kwavile mmehitaji niwasumbue mda huu subirini sasa”
Neema akatoweka na kuwashtua zaidi ila kila walipojaribu kuinuka ili waweze kukimbia miguu yao ilikataa kuinuka kabisa na ilionekana kuishiwa nguvu kila muda unavyoenda mbele.
Gafla wote wakapitiwa na usingizi na hakuna aliyejua tena kinachoendelea pale sebleni.
Ule usingizi ulimpeleka Sophia sehemu nyingine kabisa, alikuwa mahali na kuwaona wale watoto watatu ambao huwa anawaona kwenye ndoto huku mmoja mmoja akimuaga na kuondoka. Sophia aliwaangalia wale watoto na kutabasamu kisha akawaambia,
“Mmerudi tena kwenye maisha yangu, nitafurahi sana. Je mmerudi?”
Hawa watoto wakatikisa kichwa na kumfanya Sophia aseme tena,
“Tafadhali msinifanyie hivyo, najua nyie ni wanangu naomba mrudi katika maisha yangu. Nawapenda sana.”
Ila hawa watoto wakapotea kisha akatokea yule mtoto waliyemuokota na kutabasamu ila Sophia alikunja sura kisha huyu mtoto akamwambia,
“Kuna kitu nitakufanyiaa na kamwe hutokuja kukisahau katika maisha yako”
Sophia akauliza kwa hamaki,
“Kitu gani hiko?”
Huyu mtoto akacheka sana, kisha akamwambia tena,
“Subiri utakiona, najua kitakuumiza sana maisha yako yote ila ndio nitakuwa nimeshakifanya tayari”
Sophia akapatwa na uoga huku akihitaji kufahamu kuwa ni kitu gani anachoambiwa kuwa atafanyiwa, ila yule mtoto akatoweka mbele yake na hapo ukawa mwanzo wa kushtuka kwa Sophia.
Ibra na Siwema walikuwa hawajitambui pale chini, hivyo Sophia alianza kwa kuwashtua ili nao waamke ila hakuweza kumuamsha hata mmoja kati yao na alipojaribu tena kuinuka hakuweza kabisa kwani miguu yake ilijawa na uzito sana. Wakati akijishangaa pale, ilikuja Neema huku akitabasamu na kumuangalia Sophia, kwakweli kwa wakati huu Sophia alikuwa amejawa na uoga uliopitiliza kwani hakujua hatma ya maisha yake, Neema alianza kumwambia Sophia
“Unajua nini Sophia, mwanzoni nilikupenda sana kwani nilikuona ni binti mpole na mwenye huruma ndiomana ulipopata mimba nilijitolea kukusaidia kazi mbali mbali kwa huruma yangu juu yako. Nilijitolea kukuandalia chakula kizuri cha kukupendeza kwaajili ya mtoto wako ila mlinikera sana wewe na mumeo siku yule mtoto mliyemkuta njiani halafu akapanda kwenye gari yenu, mlimtoa kwa nguvu na kumtupa. Yule mtoto alikuwa ni mimi, kwavile mliniudhi ndiomana nikapanga njia ambayo nyie mngenikaribisha wenyewe ndani kwenu na ndivyo ilivyokuwa, mlinikuta njiani na mkanikaribisha wenyewe nyumbani kwenu. Sikutaka muwe na mashaka na mimi ila kutwa kucha kutaka kunichunguza ndio kilichowaponza, nikaja tena kwa njia ya mtoto pia ukagoma kuninyonyesha”
Sophia akashtuka na kuuliza,
“Inamaana yule mtoto ni wewe?”
Neema akacheka kisha akamuuliza Sophia,
“Ulidhani yule mtoto ni nani?”
“Sijui, sasa ni maziwa gani uliyokuwa unanyonya kwangu?”
“Mimi sikuwa nikinyonya maziwa, nilikuwa nanyonya damu kwani damu yako inanipendeza sana ni tamu kwangu na inanipa afya”
“Sasa si inamaana ulikuwa unanimaliza damu? Je nimewezaje kuendelea kuishi hadi leo?”
“Mbona mbu nao huwa wanawanyonya damu nab ado mnaendelea kuishi!”
“Kwani wewe ni nani?”
“Mimi ni Neema”
“Ndio wewe ni Neema, ila ni mtu wa aina gani?”
Neema akacheka sana kisha akamwambia tena Sophia,
“Usitake kunijua kwa undani zaidi kwani unaweza kushindwa kuendelea kuishi na mimi lengo yangu si kuwaua”
“Ila lengo lako ni nini?”
“Lengo langu ni kuwatesa”
“Na kwanini unatutesa jamani?”
“Kilichowaleta humu ndani ndio kitawaambia kwanini nawatesa”
“Na kama lengo lako si kutuua, mbona wanangu mmewaua?”
“Sophia, Sophia sina muda wa kuendelea kukujibu zaidi ngoja niwaamshe wenzio ili mjaribu kupanga mipango ya kunitokomeza”
Neema akacheka sana na kutoweka, muda kidogo Siwema na Ibra walishtuka kutoka kwenye ule usingizi mzito waliokuwa wamelala.
Siwema alikuwa akijifikicha macho, Ibra nae vivyo hivyo huku kila mmoja akijaribu kurudisha kumbukumbu ya matukio yaliyowapata kabla ya kupatwa na usingizi na kila mmoja akakumbuka kila kilichotokea. Siwema akajikuta akitokwa na machozi tu,
“Jamani nisaidieni tafadhali niweze kutoka humu ndani kwenu, kwani na mimi nimefanyaje jamani?”
“Pole dada, hata sisi tunatamani kutoka hivyo hivyo ila hatujui tunatokaje dada yangu”
“Kumbukeni nina familia jamani, yani mambo yaliyonipata usiku kweli ndio yanaenda kunipata tena dah! Nisaidieni nitoke jamani”
Wote walikuwa kimya kwani kiukweli hakuna aliyekuwa na uwezo wa kufanya chochote ili waweze kutoka kwani kila mmoja ni kama alikuwa gizani hata miguu yao bado haikuweza kuinuka na kikubwa zaidi ni njaa kwani kila mmoja alikuwa na njaa ya kutosha ukizingatia ni tangu walipokula jana yake, na wakiangalia hali ilivyo ilikuwa ikionyesha kuwa usiku nao ulikuwa unaingia. Siwema akawauliza tena,
“Kwani nyie huyu Neema mlimfanya nini?”
“Hatujamfanya chochote ila tunashangaa kwanini anatufanyia hivi”
“basi nisaidieni mimi nitoke”
Muda ulipita na kimya kikatanda, Siwema alipoona vile akaamua kujikongoja kwa kujisukuma hadi mlangoni aangalie uwezekano wa kufungua mlango ili aweze kutoka. Aliweza kufika mlangoni na akaanza kujitahidi kuinuka hadi kufanikiwa kufungua mlango, ila mlango ule ulipofunguka aliingia Neema huku akicheka sana na kumuuliza Siwema,
“Eeeeh unaenda wapi? Tena wewe una kiherehere sana, nilijua tu ipo siku utaingia kwenye anga zangu ndiomana nilikuwa nikikuangalia tu. Unafikiri ni rahisi hivyo kutoka humu ndani? Labda niamue mimi mwenyewe, na ili niamue muweze kutoka mnatakiwa kufanya kitu kimoja nitakacho waamrisha”
Ibra alijibu huku akiwa ametazama chini kwani kiukweli alishatambua kuwa Neema hakuwa binadamu wa kawaida kwahiyo aliogopa hata kumtazama usoni,
“Tupo tayari”
“Kuna chakula mezani, nitakapo waruhusu kuinuka nahitaji wote muelekee pale mezani na kula kile chakula”
Hakuna aliyepinga ukizingatia njaa ziliwashika sana, Neema kama alivyopanga akatoa amri moja na wakaweza kuinuka kutoka pale chini kisha kuelekea mezani, aliyekuwa wa kwanza kukipakua kile chakula na kuanza kukila alikuwa ni Ibra ila Siwema na Sophia waliogopa,
“Jamani, tuleni hiki chakula tuepuke matatizo. Kwani tukila kuna tatizo gani? Hebu tuleni jamani, sitaki kuona mkiumia ndugu zangu”
Siwema nae akaamua kupakua kile chakula na kuanza kukila kwani alikuwa na lengo kubwa sana la kurudi nyumbani kwake, kwahiyo alikula kile chakula ukizingatia na njaa yake basi akala sana tu. Ila tatizo lilikuwa kwa Sophia kwani hakutaka hata kukionja kile chakula na kujihisi kuwa atarudishwa nyuma alikotoka ambako hakutaka kurudi tena.
Walipomaliza kula walirudi na kukaa kisha kupitiwa na usingizi kasoro Sophia, kisha Neema akasogea na kumwambia Sophia
“Si umegoma kula eeeh! Utakula jeuri yako”
Neema akapotea, Sophia akajaribu kuwaamsha wenzie lakini hawakuamka na kumfanya azidi kupatwa na uoga wa maisha yale. Ila kwavile yeye alikuwa na maumivu ya miguu kutokana na ile ajali ikawa ni ngumu kwake kuweza kutembea mwenyewe mpaka asaidiwe, na wa kumsaidia kutembea mwenyewe ndio huyo amepatwa na usingizi na hata kushtuka hashtuki.
Muda kidogo Sophia akaanza kujihisi maumivu kwenye miguu na yote ni sababu ya kutokunywa dawa ambazo zilikuwa chumbani, ila kutokana na majanga yaliyowakumba sebleni kwa siku hiyo hakuweza kunywa dawa kabisa kwahiyo muda huu miguu ilikuwa ikimuuma sana na kumfanya hata alie lakini hakupata msaada kwavile hawa wa kumuhudumia walikuwa hoi na usingizi.
“Nitafanya nini mimi jamani, miguu inaniuma sana”
Kidonda kilikuwa kimevunda, alitaka kujaribu kujisukuma ili aweze kwenda kuchukua dawa ila kila alipojisukuma ndio maumivu nayo yalivyomzidia na kumfanya akose raha kabisa huku machozi nayo yakizidi kumtoka.
Giza liliingia na hapakuwa na mtu wa kuwasha taa kwavile Ibra na Siwema walikuwa hoi na usingizi, kuna upande mwingine war oho yake Sophia ukamlaumu kuwa kwanini hakula kile chakula usikute asingepata mateso yale ya kusumbuka na kidonda, huku upande mwingine ukimsifu kwa ujasiri wake kwani alihisi kile chakula cha Neema ndio kilichokuwa na mtindo wa kuwavuruga akili, ndani palikuwa na giza sana hadi kuanza kutisha mara akasikia sauti ya chura na kumfanya ashtuke sana huku akijiuliza kuwa chura ametokea wapi mule ndani kwakweli hakupata jibu ila uoga ulimjaa mwili mzima, huku akitamani nay eye apitiwe na usingizi ila usingizi haukuja kabisa na kujikuta akichanganyikiwa zaidi.
Usiku wa manane Ibra alishtuka na Siwema nae alishtuka na kuogopeshwa na lile giza walilolikuta ambapo Ibra akainuka na kujikongoja taratibu akitafuta sehemu ya kuwashia taa na alipopapata akawasha ile taa ambapo iliwaka ila walichokiona mbele yao baada ya taa kuwaka kiliwaogopesha zaidi kwani mbele yao waliona jeneza likiwa limepambwa kwa mauwa. Hakuna aliyepata ujasiri wa kuinuka na kwenda kuchungulia kwenye lile jeneza kuwa kuna nini kwani kila mtu alikuwa amejawa na uoga uliopitiliza.
Wakamshtua Sophia aliyekuwa akilia, ambapo nay eye alipoona lile jeneza alishtuka sana na ndipo hofu ilipomjaa zaidi ya mwanzo,
“Jamani tunakufa, tunakufa jamani. Tutafute msaada”
“Tutapata wapi msaada?”
“Tutoke nje, tutapata msaada tu”
Siwema alikuwa wa kwanza kuinuka na kwenda kufungua mlango ili atoke ila alichokutana nacho mlangoni kilimshtua zaidi na kumrudisha nadani kwa kasi ya ajabu,
“Vipi tena Da’Siwema?”
“Hamuwezi kuamini, hapo nje kwenu yamejaa makaburi”
“Makaburi?”
“Ndio makaburi”
Ibra akajivika ujasiri na kujaribu kwenda kuchungulia nje ambapo naye alirudi ndani kwa haraka,
“Yamejaa makaburi kweli, tutafanyaje jamani?”
“mambo haya yanamaana gani jamani?”
“Hakuna anyejua hapa, sasa tutafanyaje?”
Mara wakaona lile jeneza likifunguliwa, hapo sasa hakuna aliyeweza kustahimili kwani walijikuta wote wakizimia hata Sophia ambaye mwanzo hakulala ila hapo alizimia.
Ilikuwa ni karibia panakucha ambapo Ibra alishtuka mapema sana na kumshtua mke wake ambaye alishtuka pale pale aliposhtuliwa na Siwema vivyo hivyo ila muda huu hapakuwa na chochote pale sebleni palikuwa kimya kabisa, Siwema alikuwa wa kwanza kuongea kwa muda huu
“Jamani kwani mimi nimepatwa na nini jamani mpaka siwezi kwenda nyumbani kwangu!”
“Jaribu kutoka muda huu ila ukifanikiwa kufika nyumbani kwako tafadhari tupatie msaada maana sijui hata na sisi tunatokaje humu”
Sophia nae akaongea,
“Ila kama Da’Siwema atafanikiwa kutoka inamaana na sisi tunaweza tukatoka pia”
Basi hawakutaka kupoteza muda, ndipo Siwema alipoinuka na kuweza kufika mpaka mlangoni akafungua mlango na kutoka nje ambapo hakutaka hata kugeuka nyuma. Aliondoka kwa kasi ya ajabu hadi getini na kutoka nje kabisa ila pale nje alikutana na Neema ambaye alimwambia,
“Iwe mwanzo na mwisho kujishughulisha na mambo ya nyumba hii, ukiwa kiburi nitakuja kukukomesha nyumbani kwako. Haya potea”
Yani siwema alikimbia kama chizi na hakuangalia nyuma tena.
Ibra nae akajaribu kuinuka na kumkongoja mkewe ili waweze kutoka ila walishtukia kama mtu akiwasukuma na kuwakalisha chini.
Kisha akaona Sophia akisukumwa zaidi na kulazwa kwenye kochi ila aliyekuwa akifanya hivyo hakuonekana kabisa, Sophia akaonekana akijinyonga nyonga tumbo huku pale chini damu zikitapakaa.
Itaendelea kama kawaida…….!!!!!!!!
Toa maoni yako mdau.
No comments:
Post a Comment