Ibra akamuinua mkewe kwa nguvu na kumpakia kwenye lile gari, ila baada ya kupanda tu wote wakashangaa kwani yule dereva wa mwanzo alikuwa mwanaume na mara hiyo hiyo akawa mwanamke. Wakati wakishangaa mara lile gari liligeuka na kuwa jeneza.
Hakuna aliyeweza kustahimili wakajikuta wakianza kupiga kelele lakini hakuna mtu yeyeto aliyejitokeza kuwapatia msaada na kufanya wazidi kushikwa na uoga tu, wakahisi kama kuna mtu pembeni yao kwenye lile jeneza kwani walikuwa wamelazwa kabisa, Ibra akajaribu kuangalia ni kweli akaona mtu amewekwa pamba puani na mdomoni kwa maana kwamba mtu huyo alikuwa ni marehemu. Hapo ndio uoga uliwazidi maradufu na kujikuta wakitetemeka kupita maelezo ya kawaida huku kila mmoja akishindwa kustahimili hali ile. Kwa uoga waliokuwa nao wakajikuta wamezimia.
Wakati wamezimia, Ibra alikuwa akijiona kwenye eneo la tofauti kabisa, kwani muda huu alijiona yupo kwenye jeneza na anaenda kuzikwa, nke aliwasikia watu wakizungumza,
“Hivi imekuwaje huyu hadi amekufa?”
“Alikuwa akitoa mimba, sasa kwa bahati mbaya ndio huyo amekufa”
“Kheee jamani masikini, si bora angejizalia tu loh!”
“Yani nasikia aliyempa mimba aliikataa mimba ile ndiomana akaamua kuitoa ila mweisho wa siku ndio hiyo imempelekea kwenye mauti”
“Dah! Wanaume ni viumbe wabaya sana, ona sasa kasababisha dada wa watu kujiua”
Ibra akiwa mule kwenye jeneza akawa najiuliza kuwa imekuwaje chanzo cha kifo chake ni kutoa mimba ilihali yeye ni mwanaume na hawezi kubeba mimba, na vipi wasemwe wanaume ni watu wabaya wakati nay eye ni mwanaume? Akaendelea kusikilizia, na akawasikia kuwa wameshafika makaburini sasa wanataka kumzika huku vikisikika vilio kutoka kwa watu mbali mbali. Mara aliona kamavile jeneza limeshashushwa kwenye shimo kisha akasikia akianza kumwagiwa mchanga, Ibra akaogopa sana kuona vile kuwa anataka kuzikwa, akajikuta akipiga kelele kwa nguvu sana.
“Jamani msinizikeeeeeee……….”
Akajikuta akishtuka huku akiangaza macho huku na kule, akashangaa kuona watu wengi sana wamejaa na moja kwa moja akahisi kuwa watu hao wanataka kumzika kwahiyo Ibra aliinuka pale na kuanza kukimbia, wale watu walijaribu kumkimbiza bila ya mafanikio na kuamua kumuacha atokomee tu.
Mahali pale alibaki Sophia sasa huku akiwa amezungukwa na watu wengi sana, ambapo kuna wengine waliamua kumsaidia kunyanyuka na kwenda nae pembeni wakitaka kujua kilichompata ilihali hata yeye mwenyewe alihitaji kujua kilichotokea hadi yeye kuwa pale alipozungukwa nao, aliwauliza watu wale kwa mshangao,
“Kwani nini kimetokea kwangu?”
“Tumekukuta hapo pambezoni mwa barabara, wewe na yule kijana aliyekimbia mlikuwa hamjitambui kabisa ndipo tukaamua kuchukua maji na kuwamwagia ili mzinduke ila cha kushangaza yule kijana alipozinduka alipiga kelele kwa nguvu kuwa tusimzike kisha akaanza kukimbia na tumejaribu kumkimbiza bila ya mafanikio. Kwani nini kimewapata?”
“Kwakweli hata sijui yani sijui kabisa”
“Je yule kijana unamfahamu?”
“Ndio ni mume wangu”
“Dah! Pole, sana. Eeeh tukusaidiaje sasa, tukupeleke hospitali au?”
“Mi nitafurahi kama mkinipeleka nyumbani kwetu jamani maana hata sijui kama wanajua ninavyoendelea”
“Sawa, basi utatuelekeza huko kwenu tukupeleke ila nadhani itakuwa vyema kama ukila kabisa”
Kisha watu hawa wakamletea Sophia chakula ambapo alianza kula kama anakimbizwa kwani alikuwa na njaa sana, kila mmoja alimuhurumia kwani alionekana wazi kuwa ana matatizo.
Sophia alipomaliza kula sasa aliweza kukumbuka matukio yaliyompata mwishoni kabla ya kukutwa wakiwa wamezimia na mume wake, akakumbuka kuwa mwishoni walipanda gari ya kukodi na kujikuta kwenye jeneza badala ya gari. Sasa akafikiria ukarimu wa watu hawa waliowasaidia kama ni watu kweli au ni kati ya yale mauzauza yakiendelea, akawa anajiuliza moyoni tu,
“Hivi hawa ni watu kweli wameamua kunisaidia au ni kati ya mauzauza jamani?”
Wakati akiwaza hayo, kuna mmoja alimsogelea Sophia na kumwambia kwa sauti ya chini kabisa,
‘Hawa si watu kama unavyofikiria, yani watu kweli ni wale tuliwaacha nje ila hawa humu si watu hakuna mtu hapa”
Sophia akaanza kushikwa na uoga kwani kila muda unavyozidi kwenda mbele ndivyo anavyoona kuwa maisha yake yapo hatarini,
“Sina makosa mimi, nisameheni”
“Usipige kelele Sophy, kuwa mpole mimi nitakusaidia”
“Nitaamini vipi kama utanisaidia ikiwa na wewe ni mmoja wao?”
“Sikia nikufundishe kitu, wakikwambia uwaelekeze kwenu ili wakupeleke waambie naomba nikae kae hapa kwa muda halafu ndio nitaenda huko kwetu maana sina amani nako. Na wakikuuliza kama kuna jambo lolote unakumbuka kuwa lilikutokea kabla ya kupoteza fahamu waambie kuwa hukumbuki chochote umesikia?”
Sophia akamuitikia huyu mtu ambaye alionekana ni mtu wa kawaida tu kama wale wengine ingawa mwenyewe alidai kuwa wale si watu wa kawaida. Kisha huyu mtu akamwambia tena Sophia,
“ Na ukiona chochote mbele yako usishtuke hatakama ukiona jeneza hata usishtuke yani chukulia kawaida tu maana kushtuka kwako kutakupoteza”
Sophia akaitikia huku akijiuliza mahali atakapopata huo ujasiri wa kutokushtuka na uoga aliokuwa nao kwakweli alihisi kama kuchanganyikiwa sasa. Yule mtu akaondoka na kumuacha Sophia akiwa amebaki mwenyewe.
Muda kidogo wakaja wale watu waliomsaidia Sophia ambao walikuwa kama watano hivi ukiongeza na yule mmoja aliyekwenda kuongea na Sophia peke yake, wakaanza kumuuliza maswali Sophia,
“Je unakumbukumbu zozote za kilichokupata hadi tukakukuta pale?”
“Hapana sikumbuki chochote”
Sophia alijibu huku akiwaza kuwa huenda yule mwingine ndio mbaya, pengine hataki hawa binadamu waujue ukweli ila akajipa moyo tu kwani hakuwa na chochote cha kufanya ukizingatia mazingira yale alikuwa hayafahamu na wala wale watu waliomsaidia hakuwafahamu kwahiyo cha msingi na muhimu ni kuwa mpole tu. Kisha hawa watu wakamuuliza tena,
“Vipi tukupeleke kwenu? Tuelekeze ili tukupeleke”
“Nawaombeni nikae hapa kidogo, msinipeleke kwetu kwanza maana sikumbuki chochote labda mambo mabaya yalinipatia huko kwetu”
“Mmmh pole sana, kwahiyo hutaki kwenda kwenu kabisa?”
“Nitaenda tu, ila kwasasa nawaomba kwanza akili yangu ikae sawa maana haipo sawa na sina imani na nyumbani kwetu”
Hawa watu hawakuongea zaidi ila walimuacha Sophia pale na kutoka katika eneo lile, muda kidogo Sophia aliona kundi kubwa la watu likiingia mule ndani huku wakilia na kuomboleza, wakaonekana vijana wakiwa wamebeba jeneza. Hofu ikamshika Sophia ila akakumbuka maneno ya yule mtu kuwa asistuke wala nini kwahiyo akajipa moyo na kutulia, wale watu wenye jeneza walikuja na kukaa karibu yake huku wakilia sana ila Sophia alikuwa ametulia tu na ili kujiepusha kushtuka akaamua kuhamisha mawazo yake kutoka eneo hilo yani ingawa alikuwa pale akiwatazama alkini mawazo yake hayakuwa hapo kwabisa.
Muda mrefu kidogo ukapita huku wale waomboleaji wakiendelea na kazi yao ya kuomboleza na wengine kuendelea kulia huku wakiimba nyimbo, muda kidogo akasikia wakizungumza
“Tutaenda kumzika mpendwa wetu Sophia kwenye yale makaburi ya juu”
Alitaka kushtuka ila akasizi kidogo na kutulia ili ile hali isimsumbue zaidi, akawaona wengine wakizidi kulia kisha lile jeneza likabebwa na kutolewa mahali pale kisha kimya kikatawala halafu wakaja tena wale watu watano. Mmoja akamuuliza Sophia,
“Mbona unaonekana kuwa na mawazo sana?”
“Ni kweli nina mawazo sana ila ninachowaza ni kujaribu kukumbuka kilichonipata”
“Hujaweza kukumbuka chochote?”
“Sikumbuki kitu”
“Je hujaona watu humu ndani wakiwa wamebeba jeneza?”
“Saa ngapi hao watu wameingia?”
“Kweli inaonyesha kuwa na mawazo sana”
Yuel aliyekuwa akimtonya Sophia mwanzoni kabisa alionekana kutabasamu na ilionyesha wazi akifurahia majibu yale ya Sophia, wenzie wakamuangalia na kumuuliza
“Mbona unafurahi sasa?”
“Sifuwahi kama mnavyofikiria ila ananishangaza sana huyu binadamu”
“Kivipi?”
“Anakosaje kumbukumbu jamani?”
“Kwahiyo tufanyeje?”
Mmoja akaonekana kuwatahadharisha wenzie,
“Jamani taratibu, asije kugundua”
Kisha wakaondoka tena na kumuacha Sophia eneo lile, moja kwa moja Sophia aliweza kuelewa kuwa hawa hawakuwa binadamu wa kawaida ila tu hakuelewa kuwa wamepanga kumfanyia jambo gani. Akatulia sasa huku akijiuliza zaidi kuwa hatma yake itakuwa ni nini maana hakuelewa mwanzo wala mwisho.
Wakati akitafakari, yule mtu wa mwanzo akamjia tena Sophia na kuzungumza nae kwa sauti ya chini kabisa.
“Usiogope chochote, kwa hili mimi nitakusaidia”
“Utawezaje kuwasaliti wenzio si watagundua?”
“Wee jiulize tu, nawezaje kuja hapa na kuzungumza na wewe bila ya wao kujua. Nakuhurumia sana Sophia, adhabu ulizopata zinatosha kabisa wala hazistahili kuendelea juu yako na wala sioni kosa lako ndiomana nasema nitskusaidia”
“Nitashukuru sana ukinisaidia”
“Usijali kuhusu hilo kabisa, amini kuwa nitakusaidia Sophia”
Kisha kimya kidogo kikatawala, na huyu mtu akaanza tena kwa kumwambia Sophia kuhusu mpango aliopangiwa sasa,
“Wanahitaji kukupeleka porini, kwahiyo wakija hapa na kukwambia kuwa twende nje ukapunge hewa unatakiwa ukatae”
“Wakinilazimisha je!”
“Tambua kwamba uwezo wa kukulazimisha kufanya chochote kile wanao ila kwasasa inatakiwa ukubali mwenyewe kwa hiyari yako kwani lengo kubwa ni kukumaliza kabisa na ili kukumaliza lazima wewe ukubali mwenyewe kwa hiyari yako”
Sophia akabaki kushangaa tu na kujiuliza kwanini wanahitaji kummaliza kabisa na kwanini anatakiwa kukubali mwenyewe kwa hiyari yake, huyu mtu akamjibu Sophia,
“Iko hivi, mfano ukiwa umelala gafla kwenye ndoto akatokea nduguyo aliyekufa miaka mingi iliyopita na kukuomba umfate kwani alipo ni pazuri sana, unapokubali ni kwamba umeridhia kwa hiyari yako na mara nyingi hazitapita siku nyingi sana utakuwa umekufa kweli na kumfata ndugu yako huyo ila ukikataa ndio pona yako hata kama ulianza kuumwa utashangaa unapona sababu ya kukataa kuongozana nae. Kuna vitu huwa tunafanya kwa kulazimisha ila vingine inatakiwa muhusika akubali mwenyewe kwa hiyari yake, na kwa hali iliyofikia kwako kwasasa unatakiwa ukubali kwa hiyari yako mwenyewe ili tukumalize kabisa”
Sophia akatulia kimya kwa muda na kujikuta akikumbuka stori za zamani alizowahi kuambiwa na mama yake, akakumbuka kuwa mama yake aliwahi kumsimulia kuhusu kifo cha mamake mdogo amabpo inasemekana aliitwa na kaka yao ambaye ni mjomba wake marehemu. Mamake mdogo kipindi hiko alianza kuumwa taratibu na baada ya kusimulia huo mkasa wa kuitwa na kukubali alikufa baada ya siku mbili, mama yake alikuwa akiwasimulia huku akiwasisitiza kuwa wasipende kuitika wakiwa ndotoni na wasikubali chochote kama kuitwa na marehemu wakiwa ndotoni kwahiyo akahusisha matukio haya na alichokuwa akiambiwa na huyu mtu. Kimya kilitawala kwani huyu mtu alihitaji Sophia aweze kutafakari, kisha akaendelea kumwambia.
“Chochote watakachokwambia uwe unakataa kabisa yani usikubali chochote kile, halafu itatubidi twende kwa mkuu kushtaki kuhusu jambo hili na kuomba ruhusa ya kutumia nguvu. Wakati wa kwenda kwa mkuu mimi nitabaki hapa na kudai kuwa natakiwa kukulinda kwani bado hatuna imani na eneo hili kisha wao wataondoka. Hapo nitakusaidia kurudi kwenu na tafadhari nikikufikisha njia ya kwenda kwenu usigeuke nyuma”
Huyu mtu akaondoka na kumuacha Sophia peke yake akiendelea kutafakari kwani alikuwa kama mti asiyejielewa kabisa kwa wakati huo na alionekana wazi kutokujua cha kufanya.
Wakati Sophia amekaa hapo, wale watu watano wakaja tena huku wakiwa na zile hoja alizoambiwa na yule mmoja wao.
“Sophia, tunahitaji twende wote nje ukapunge upepo. Tafadhari inuka twende”
“Hapana jamani, niacheni kwanza hapa”
“Kwanini lakini Sophia? Hutaki kuona hali ya nje? Hutaki kuona kama ni usiku au mchana?”
“Mi najiona salama zaidi nikiwa hapa, tafadhari niacheni hapa”
“Basi simama kidogo ujinyooshe”
“hapana, hata sijisikii uchovu wa kujinyoosha”
“Hata kusimama kidogo hutaki jamani?”
Sophia aligoma kabisa na aliona wazi sura za hawa watu zikijawa na hasira kwa kugoma kwake na walionekana wazi wakitamani kumlazimisha ingawa hawakufanya hivyo, wakainuka na kutoka nje kisha kimya kirefu kikatawala.
Muda kidogo alirudi yule mmoja na kumwambia Sophia,
“Haya sasa wameondoka, rudi nyumbani kwenu. Fumba macho”
Sophia akafumbua macho na gafla akajiona kuwa amesimama mahali, huyu matu akamwambia Sophia,
“Fumbua macho”
Sophia akafumbua na kujiona yupo kwenye njia ya kuelekea nyumbani kwao, huyu mtu akamwambia tena Sophia
“Kumbuka usigeuke nyuma, hata ukisikia mtu anakuita usigeuke nyuma. Hakikisha hadi unaingia ndani kwenu bila kugeuka nyuma, yani kosa la kugeuka nyuma utajutia maisha yako yote kupita unavyojutia sasa. Kwaheri”
Huyu mtu akatoweka kisha kimya kikubwa sana kikatawala kwenye eneo lile ambapo Sophia alisimama kwa muda kwanza.
Kisha Sophia akaanza kusonga mbele kurudi kwao, ni kweli akasikia sauti nyingi zikimuita kwa nguvu ila Sophia hakugeuka nyuma kabisa hadi alipofika nyumbani kwao.
Alishangaa pale kwao kukiwa kuna watu wengi sana, na sauti zilisikika wakilia na kuomboleza huku wakitaja jina lake.
Itaendelea kama kawaida………..!!!!!!!!!
Toa maoni yako mdau.
No comments:
Post a Comment