Friday, 12 August 2016

MWENYEKITI WA CCM MH DR JOHN MAGUFULI

MWENYEKITI WA CCM MH DR JOHN MAGUFULI

MAPOKEZI KATIKA OFISI NDOGO YA MAKAO MAKUU YA CCM, LUMUMBA

12 .8.2016

DONDOO


#Ninawashukuru wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM kwa kunipa uwenyekiti wa chama chetu. Huenda sikustahili, lakini walinichagua. Ninwashukuru sana.

#Nitatumia akili zangu na nguvu zangu zote kuwafanyia kazi watanzania kwa bidii.

#Chama cha Mmapinduzi ndio chama tawala...kipimwe ndani ya miaka mitano.

#Tumeamua kufanyakazi. Nataka niwahakikishie watanzania wenzangu...tumepanga kufanya kazi.

#Katika CCM...tumepanga kujisahihisha...

#CCM ilianza kupoteza dira. Chama kilianza kuwa cha matajiri...

#Nimejipanga kufanya kazi kwa kushirikiana na watanzania wote.

#Nataka nijenge chama chenye maadili nazuri kama alivyokiacha Mwalimu Nyerere. Nataka nirudishe heshima ya chama hiki. Ninawaomba wana ccm wenzangu...wakati ninafanya kazi ya kurudishnidhamu ya chama mnivumilie. Maananitakapoamua kunyoosha, nikikunyookea...

#Natakaccm mpya

#CCM imeundwa na wanachama wa kawaida...kamwe sitakubali watu wanaotaka uongozi ndani ya chama watumie pesa...

narudia kusema...

#Yeyote mwenye uwezo wa kuongoza mwakani aombe uongozi. Atakayetumia rushwa ajuehatarudi
#Ninataka ccm mpya. ninataka Tanzania mpya. Twende na kuhakikisha tunaondoa kero za wananchi wetu.

#Ilifikia mahali watoto wa maskini wanarudishwa nyumbani kwa kukosa karo...ndio maana sasa tumeamua kutoa elimu ya sekomdari bure.

#Sasa nataka niwaeleze,   msiangaike kunywa vidonge vya majira, zaeni...fyatueni watoto kwasababu watasoma kuanzia la kwanza hadi sekondari.

#Hakuna mtoto atakayerudishwa nyumbani eti kwa kukosa ada, awe CCM, UKAWA, CUF...

#Tutaendelea kusimamia nidhamu ndani ya Serikali

#Mapato: Makusanyo yamapato yameongezeka.

#Nataka niwahakikishie, tumejipanga kufanya kazi kwa niaba yamaskini wa nchi yetu. Mimi mwenyewe ni mtoto wamaskini.

#Ninataka tujenge nidhamu ndani yaSerikali

#Tupo kwa ajili ya watu wa kawaida

#Akina mama lishe, machinga wasibughudhiwe katika maeneo yao

#Watengenezeeni mazingira mazuri ya watu hawa kufanya biashara katika maeneo yao.

#Tujenge mazingira ya kuwasaidia maskini  hawa kufanya kazi zao vizuri.

#Ninaitaka Tz ambapo maskini anakuwa na haki sawa na matajiri...sote tumeumbwa na Mungu mmoja

#Endeleeni kumtanguliza Mungu na tuilinde amani yetu.

#Tunataka kulifanya jiji la Dar Es Salaam liwe jiji la kibiashara ndio maana sisi tumeamua kupisha kwenda Dodoma

#Nataka kuwahakikishia kuwa viwanda vinakuja...ajira zitapatikana hasa kwa watanzania wanyonge.

#Tunataka tujenge reli. Vijana mkatafute kazi kule reli inakopita...

#Mwezi ujao ndege mbili zinaingia nchini.

#Tutaboresha na viwanja vya ndege.

#Maji Dar Es Salaam yatakuwa ya uhakika.

#Afya: Tunataka kila mtanzania akienda hospitali apate dawa. Hiyo ndio Tz mpya ninayoitaka...nimecaguliwa na maskini lazima niendane nao.

#WanaCCM tembeeni vifua mbele...mambo yatakuwa mazuri tu.

#Ndio maana nataka niyafuatilie haya mafisadi yaliyobaki ndani ya CCM...mengine tayri  yalisha kimbia.

#Mapato: mfano mapato ya majengo ya UVCCM, UWT, WAZAZI yanakwenda wapi. Nitayachambua haya mpaka kieleweke...nitalala nao mbele.

#Inawezekana kuja kwangu ndani ya CCM wengine hawatafurahi...lakini tutajenga upya chama chetu.

#Haiwezekani kama kikubwa hiki, kila tukitaka kufanya uchaguzi tukaombe hela kwa matajiri. Haiwezekani.

#Nataka chama kilicho okoka... Nataka CCM iendelee kutawala milele.

#Kwanini chama kikubwa hiki kama CCM hakina hata TV yake?

#Nataka CCM yenye lengo la kutawala na wala sio CCM yenye kubembeleza kutawala.

#Watanzania hasa vijana, ilifika mahali wakapoteza matumaini kwa kutawala. Tutafufua mtumaini ya vijana.

#Kuna wengine wanasema kuhamia Dodoma haiwezekani. Mbele ya Magufuli itawezekana.

#Nilishasema ndani ya miaka minne na miezi minne iliyobaki, Serikali yote itakuwa imehamia Dodoma.

#Kuhamia Dodoma hakuna mjadala.

#Mh Kinana nakupongeza sana. Umekijenga chama. Nitaendelea kujifunza kutoka kwako.

#Ninamshukuru sana Mh Jakaya Mrisho Kikwete. Nitaendelea kuchote busara kutoka kwake na viongozi waliomtangulia.

No comments:

Post a Comment